0



Wimbo mpya wa ‘Marry You’ wa Diamond aliomshirikisha Ne-Yo kuchezwa kwa mara ya kwanza kupitia kituo cha radio cha Uingereza, Capital Xtra Radio ya nchini Uingereza.
13269419_1109188999169399_1336650774_n
Kupitia mtandao wa Twitter wa redio hiyo wameandika, “*Exclusive First Play* Wow! This new @diamondplatnumz ft. @NeYocompound ‘I Will Marry You’ is big!.”
Wimbo huo ulitayarishwa na Sheddy Clever mwaka uliopita na tayari video a wimbo huo imeshatengenezwa tangu mwezi Septemba mwaka huu huko jijini Los Angeles, Marekani.
Huu utakuwa wimbo wa pili wa hitmaker huyo wa Salome kuchezwa nchini humo baada ya wimbo wa ‘Kidogo’ kuchezwa kwenye kituo cha BBC Radio 1Xtra tangu mwezi Agosti mwaka huu.

Post a Comment

 
Top