Wezake wote wakahamaki kila mmoja hakuamini kuona tukio lililopo mbele yao,Rahab akatupa shoka chini na kuwatazama wezake usoni kwa umakini
“Munacho ogopa nyinyi ni nini?”
“Ehee ahaaa hapana” Halima alijibu kwa kubabaika
“Tuutoeni sasa huu mwili”
“Tutaupeleka wapi?”
“Mimi ninaona tukodishe taksi”
“Dereva gani ambaye atakubali kubebea maiti?”
“Sasa itakuwaje?”
Wote wakakaa kimya wakitafakari ni nini cha kufanya,Fetty akawatazama wezake kwa umakini kisha akazungumza kwa sauti ya kujiamini
“Mmmmm”
“Agnes usigune unadhani kuna mtu anataka kwenda jela wakati kama huu....mimi bado ninayapenda miasha ya uraiani japo yanachangamoto kama hizi”
“Basi tuanzeni kuifanya hiyo kazi”
“Angekuwa ngombe huyu mama nahisi saa hizi si chini milioni tungekuwa tumesha pata”
“Kweli nawaambia...Huyu mama angekuwa ni ng’ombe ahaa mbona tungepata mshiko wa maana”
“Alafu si ninasikia kuna makabila wanakula nyama za watu?”
“Mmmmm kabila gani hizo?”
“Wapo ila nahisi Tanzania hakuna”
“Tanzania mbona wapo?”
“Kabila gani?”
“Wachawi”
“Jamni safari ya wapi?”
“Kuna mzungu mmoja juzi kati nililala naye yupo maeneo ya mbezi bichi twendeni kwake”
“Anna acha ushamba unataka kusema kutembea kuto huko hujaona geti kama hili?”
“Sijawahi”
“Ahee shosti nawe umezidi ushamba”
“Tuachene na hilo je hii safleti niiweke wapi kwa maana nimechoka kuibeba”
“Idumbukize hapo kwenye hayo maua”
Halima akaidumbukiza safleti kwenye maua yaliyo tengenezwa vizuri kisha wakaingia kwenye jumba la dokta Wiliam.
Dokta William alizungumza kwa Kiswahili cha kujing’ata nga’ta na Rahab akamkumbatia Dokta William na kumpiga mabusu ya kinafki kisha wakajibwaga kwenye masofa ya dhamani yaliyomo mule ndani
“Rahab ona wewe leo fanyia mimi Suprize”
“Mimi wezi saliti wewe kutokana moyo wangu penda sana wewe,shindwa hata fanya kazi kwa mambo yako ya kukatika kitandani fanya mimi Crayz”
Wote wakacheka huku wakimtazama Dokta William
“Usijali kama ni kiuno tuu utakipata leo hadi uimbe wimbo wa Taifa la nchi yako”
“Ndio kwani kuna siku ambayo nimeshawahi kukudanganya?”
“Ahhaa utafanya mimi nisirudi nyumbani maana nyinyi Afrika munajoto sana tofauti na wanawake ngozi nyeupe wao baridi sana kama amfibia(viumbe wenye asili ya kuishi kwenye maji)”
“Kuna mashaka jumba lote hili kaa mimi peke yangu tena ona raha kuona sichana rembo kama nyinyi kuja kaa na mimi nitapata burudani kedekede”
“Ombi gani?”
“Tunaomba gari yako hiyo ya UN twende nayo sehemu mara moja kisha tunarudi?”
“Mbali sana na hapa?”
“Hapana sio mbali kivile na hapa”
Rahab akawatazama wezake na wakakubaliana kwa ishara na wote kwa pamoja wakasimama na kuacha vitu vyao,Agens akaichukua safleti yenye mwili wa mama Bonge na wakaingia kwenye gari aina ya pick up Ford na wakamuomba dokta William waelekee nje ya jiji kidogo.
“Kuna mzigo tunakwenda kuutupa”
“Nini tena?”
“Ni mwi......”
“Rahab”
Fety alimzuia Rahabu hakumalizia anacho taka kukizungumza kwa maana kinaweza kikaleta mtafaruku baina yao na mzungu huyu.
Dokta William aliuliza huku akiongeza kasi ya gari hadi na kuliacha jiji la Dar es Salaam,
“Ahaa ni mzigo wa kawaida tuu mpenzi wangu wala usijali katika hilo”
“Isije ikawa dawa kulevya”
“Ahaa mpenzi wangu umeona wapi mtu akatupa dawa za kulevya wakati ni dili kabisa hilo”
“Mbona wezako kaa kimya hawapigi story”
“Ahaa sasa mimi huku Pwani kuna handaki langu kubwa kama hamtojali nyinyi kaa humo kwa siku kama mbili tatu kisha rudi mjini kwa maana pale nyumbani kwangu kesho fika wakuu wangu toka state of America sasa shindwa nyinyi juiwapi kaa”
“Ehee tena itakuwa vizuri”
“Eti warembo nyinyi mpo tayari kukaa kwenye handaki?”
“Ni wewe tu”
Maisha yakazidi kwenda mbele huku kila siku jioni Dokta William akija kuwatembelea Rahab na wezake na kuwafundisha baadhi ya mbinu za kijeshi kwani Dokta William na miongoni mwa wanajeshi wanaotegemewa sana katika jeshi la umoja wa mataifa UN.Kadri siku zinavyo zidi kwenda ndivyo jinsi Rahab,Agnes,Anna,Halima na Fety walivyo zidi kukomaa katika mafunzo ya kijeshi ambayo Dokta William aliamua kuwafundisha ili kuwatumia katika biashara zake haramu anazo zifanya akishirikiana na baadhi ya viongozi serikalini.
“Ndio”
“Sasa hapa kuna kazi moja taka nyinyi anza kuifanya kwa umakini na umahiri wa hali ya juu...”
Dokta William alizungumza huku akiwa amesimama kwenye kitambaa cheupe kikubwa huku mwanga mkali unaotoka kwenye kifaa kidogo(projectar) na kuna picha mbili za wanaume zikiwa zinaonekana kwenye kitambaa hicho.
“Dokta kwahiyo unataka sisi tuwaue hao?”
“Ndio nataka ua huyo Karim sasa hivi yeye yupo Dar kwenye hoteli Serena na huyu Mansuri yeye yupo Tanga hoteli moja itwa Tanga bich resolt”
“Samahani Dokta je hawa watu wana makosa gani hadi sisi tuwaue hilo ni swali namba moja,swali namba mbili je utatuhakikishia vipi usalama wetu na tatu malipo yatakuwaje?”
Halima akashusha pumzi nyingi huku akiwatazama wezake ambao wameridhika na kazi hiyo ya mauaji.
“Je na sura zetu tuzaziwekaje?”
“Agnes hapo mutajua ni jinsi gani ya kucheza huo mchezo wa sura zenu na hizi ndizo namba zao za simu”
Kwa mwendo wa masaa manne kutoka mkoa wa Pwani hadi Tanga ukawafanikisha Rahab na Agnes kufika Tanga na moja kwa moja wakaelekea kweneye Hotel ya Tanga beach Resolt na wakachukua chumba kimoja na kuanza kumtafuta Muntar ni wapi alipo.Wakiwa wamejipumzisha pembezoni mwa swimming pool lililopo kwenye hoteli hii wakamuona Muntar akiingia hotelini akiwa ameongozana na wapambe wake wapatao sita wanao mlinda na wanaonekana wapo makini sana kwa kila mtu ambaye anapita karibu na bosi wao.
“Nimemsoma wangu so tunalianzisha sasa hivi?”
“Hapana tutumie akili nyingi kumuua la sivyo hatuto toka salama humu ndani”
“Una wazo gani kichwani?”
“Uzuri wetu unaweza pia ukampagawisha?”
“Je ni mtu wakupenda wanawake isije tukajipendekeza ikala kwetu”
“Ngoja tuyasome mawazo yake”
Muntar aliwaamrisha wapambe wake na wakamtii na mmoja wao akanyanyuka kwenda kumfatwa Agnes kwenye eneo la kuuzia vinywaji ili kuzungumza ombi la bosi wake analo lihitaji...
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.