0
Muongozaji wa video za muziki nchini afananisha ujio wake mpya kama Nicolas Cage kwenye filamu ya ‘Ghost Rider’ na kusema moto utawaka, minyororo yenye moto itarushwa na pikipiki zenye spidi zitaunguruma !
Katika ujio wake huo mpya, Nisher ambaye kwa mwaka 2015 alikuwa kimya amedai anarudi kitofauti kabisa. Kuonesha kuwa mwaka 2016 kuwa utakuwa wa kazi tu, muongozaji huyo ameshare picha ya cover la Nicolas Cage ya Ghost Rider kuonyesha msisitizo wa jinsi mwaka huu utavyokuwa wamoto.

Mbali na Cage tofauti yao ni silaha, ambapo Nisher yake ni Kamera. Kati ya wasanii wakwanza atakaofanya nao kazi mwaka huu ni G nako na msanii chipukizi The Voice Fairy. Hivyo wapenzi wamuziki kaeni tayari kuona kasi hiyo na nguvu hiyo mpya anayokuja nayo director Nisher. All The Best!!!
-tubongetz

Post a Comment

 
Top