0
Ukumbi mpya wa CCM mkoani Dodoma.
Ukumbi mpya wa CCM mkoani Dodoma.
Baadhi ya wanachama wa CCM walijitokeza kuhudhruria uzinduzi huo.
Baadhi ya wanachama wa CCM walijitokeza kuhudhruria uzinduzi huo.
Maandalizi ya uzinduzi wa ukumbi wa CCM.
Maandalizi ya uzinduzi wa ukumbi wa CCM.
Wanachama CCM wakati wa maandalizi ya uzinduzi wa ukumbi mpya.
Wanachama CCM wakati wa maandalizi ya uzinduzi wa ukumbi mpya.
Kinachoendela Mkoani Dodoma hivisasa ni maandalizi ya uzinduzi ukumbi mpya wa CCM uliopo  njia ya kwenda chuo kikuu cha Dodoma.
Wageni mbalimbali wamehudhuria uzinduzi huu ambapo Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ndiye atakayezindua ukumbi huo lakini hadi sasa bado hajawasili katika ukumbi huu mpya na wa kisasa.
Rais Kikwete akikagua moja ya ukumbi wa kisasa uliopo katika majengo ya ukumbi mpya wa CCM mkoani Dodoma.Add caption
Kwa upande mwingine, leo  mchana kutakuwa na kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya chama cha mapinduzi ambayo nayo ni muendelezo wa vikao vya awali kuelekea mkutano mkuu.
Rais  wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete amesema kwamba  maarifa mafupi ya viongozi CCM ndio kikwazo kikubwa cha chama kushindwa kujipatia kipato kutokana na kuwa rasilimali nyingi mfu  kuliko chama chochote cha siasa nchini Tanzania ambazo hazijaweza kukizalishia chama kipato.
Kikwete amesema hayo  leo wakati akizindua jengo jipya la CCM lilipo barabara ya kwenda chuo kikuu cha Dodoma ambalo limejengwa mahusisi kwa ajili vikao vya chama  pamoja na chama kujiongezea kipato kutokana na kulikodisha jengo hilo kwa matumizi mengine.
“Ukumbi huu utatumika mara mbili tu kwa mwaka hivyo hautakaa tu usubiri vikao hivyo, utakodishwa kwa watu wengine ambao watailipa CCM”.Amesema Rais Kikwete.
Ameongeza kuwa CCM ina rasilimali nyingi ikiwemo viwanja  katika maeneo mbalimbali nchini, rasilimali hizo zimekuwa  zikigawanywa kwa viongozi wa mikoa  pamoja na mapato yake kutia mfukoni.
Ametolea mfano  jijini la Dar es salaam CCM ina viwanja taribani 420  ambavyo havija endelezwa na matokeo yake kutumika kulazia magari na  walinzi kujichukulia mapato yanayopatikana.
Amewataka viongozi wa chama hicho kuingia ubia na makampuni ya ujenzi ili  kuendeleza maeneo hayo kwa mkataba utakao zinufaisha pande zote mbili.
Amesisitiza kuwa viwanja vya CCM sasa vibadilike kutoka rasilimali mfu hadi kuwa  rasilimali  zinazotoa  na kukuza mtaji.
Ukumbi huo una uwezo wa kuchukua wajumbe takribani 3000 ukiwa na  ukumbi mkubwa pamoja na kumbi nyingine ndogo ndogo huku ukiwa na sehemu pana ya maegesho ya magari.


Post a Comment

 
Top